tiwa

Katika kuwapa pia nafasi wasanii wa Afrika, waandaaji BET Awards 2014 wamewatangaza wasanii hao kuwepo pia kwenye orodha ya watumbuizaji. Hii ni mara ya kwanza wasanii nje ya Marekani kutumbuiza kwenye tuzo hizo zitakazofanyika jijini Los Angeles tangu kuanzishwa kwa vipengele vya ‘Best International Act: Africa’ na ‘Best International Act: UK’ mwaka 2010.

Wasanii wengine watakaotumbuiza ni pamoja na K. Michelle, Mack Wilds, Mary J. Blige, Trey Songz na Jennifer Hudson. Chris Rock atakuwa host wa show hiyo.